HADITHI YA MWIZI
Habari ndugu msomaji wa blog ya “boreshamaisha”. Inawezekana
kichwa cha makala hii kimekushitua kidogo. Leo nimetamani sana tujifunze kitu
kwa kupitia wezi.
Siku moja nikiwa sokoni sehemu
wanapouza nguo za mitumba dada mmoja aliyekua akichagua nguo aliibiwa simu.
Baada ya mwizi kuchukua simu tu,
dada yule alishituka na kupiga kelele za mwizi na watu wakaanza kumfukuza mwizi
yule kwa hasira huku kila mmoja akijaribu kuokota silaha iliyopo karibu ili
amrushie mwizi yule. Lakini cha ajabu ni kwamba mwizi aliweza kuwatoroka watu
wote na kupotea vichochoroni.
Naomba uelewe kuwa nia yangu sio
kumsifia mwizi kwa kile alichokifanya lakini natamani ujifunze kitu kutoka kwa
mwizi huyu.
Kwanza mwizi huyu alijipanga
tangu muda mrefu. Yaani aliisoma picha yote ya namna wizi wake utakavyokwenda
mpaka atakapofanikiwa.
Pili mwizi huyu alikua na target.
Alifahamu tokea mwanzo ni nini alikitaka kutoka kwa nani na akajipanga
kukipata. Nadhani mwizi alitumia muda mwingi kutafuta taarifa za dada huyu. Yaani
ni aina gani ya simu anayoitumia na akiiweka anaweka wapi na pia saikolojia
kidogo ya wakati gani dada huyu anaweza kuwa amejisahau na hivyo kuweza kumwibia
kwa urahisi.
Tatu mwizi huyu alikua ni
mfuatiliaji wa hali ya juu na hakukata tamaa. Naamini kuwa alianza safari ya
kumfuatilia dada huyu kwa muda na kwa
usiri ili dada huyu asijue kuwa alikua akifuatiliwa. Hakukata tamaa ingawa
hakufahamu mwisho wa safari ya dada huyu.
Lakini nne mwizi huyu alikua
tayari kukabili hatari ya kukamatwa kama asingefanikiwa kuwaponyoka watu wote
wale. Lakini bila kujali hatari hiyo bado mwizi huyu alijikita katika kuangali
matokeo chanya ambayo kwa namna moja au nyingine yalimpa nguvu za kuweza
kufanikisha lengo lake.
Ndugu msomaji, kama kila mmoja
wetu angekua na mipango ya namna hii na kutilia umakini kwa kile anachokitaka,
na kutafuta mbinu mbali mbali za kufikia lengo alilojiwekea kama mwizi huyu
alivyofanya nadhani malengo yetu mengi tungeyafikia.
Unaweza kuwaza kuwa sio kila mara ukiweka
juhudi utafanikiwa, ni kweli sio kila mara lakini mara nyingi ukiweka juhudi
unafanikiwa. Na mara zote kama huwezi kujaribu huwezi kufanikiwa. Uamuzi ni
wako kuona kama unaweza kujitoa kwa kuweka juhudi katika lengo ulilonalo au
kuacha ili usubiri matokeo hasi.
MWANDISHI: ESTHER NGULWA
MAWASILIANO: 0767 900 110/ 0714 900 110
estherngulwa87@gmail.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni