Machapisho

Huyu Ndiye Mtu Anayeweza Kukusaidia Kutatua Changamoto Unazozipitia.

Picha
Huyu Ndiye Mtu Anayeweza Kukusaidia Kutatua Changamoto Unazozipitia. Mara nyingi binadamu tumekuwa tukilalamika kuhusu ugumu wa maisha na changamoto kuzidi kuongezeka kadiri siku zinavyozidi kwenda. Katika jamii zetu kuomba msaada ni jambo jema kabisa lakini tunachozingatia ni wapi au kwa mtu wa aina gani tunaomba msaada. Kwa wale wenye imani katika dini kila mmoja na dini yake huomba ili aweze kupata unafuu juu ya changamoto zinazomkabili. Lakini hii haimaanishi kuwa changamoto zinakwisha, ukivuka changamoto moja bado inakuja nyingine na nyingine hivyo hivyo, ilimradi maisha hayaishi changamoto. Na hii hutokea kwa watu wenye vipato vikubwa na vidogo, rika tofauti tofauti kwa ufupi kila mmoja bila kujali hadhi,muonekano au uwezo wake alionao changamoto humkabili. Wakati huu huwa mgumu lakini ugumu huu hutegemea aina ya mtu aliyepata changamoto. Kuna wengine wanaweza kupata changamoto ndogo na kuwa na uwezo mkubwa wa kuzihimili lakini wengine wakawa na changamoto ndogo ...

HADITHI YA MWIZI

HADITHI YA MWIZI Habari ndugu msomaji wa blog ya “ boreshamaisha ”. Inawezekana kichwa cha makala hii kimekushitua kidogo. Leo nimetamani sana tujifunze kitu kwa kupitia wezi. Siku moja nikiwa sokoni sehemu wanapouza nguo za mitumba dada mmoja aliyekua akichagua nguo aliibiwa simu. Baada ya mwizi kuchukua simu tu, dada yule alishituka na kupiga kelele za mwizi na watu wakaanza kumfukuza mwizi yule kwa hasira huku kila mmoja akijaribu kuokota silaha iliyopo karibu ili amrushie mwizi yule. Lakini cha ajabu ni kwamba mwizi aliweza kuwatoroka watu wote na kupotea vichochoroni. Naomba uelewe kuwa nia yangu sio kumsifia mwizi kwa kile alichokifanya lakini natamani ujifunze kitu kutoka kwa mwizi huyu. Kwanza mwizi huyu alijipanga tangu muda mrefu. Yaani aliisoma picha yote ya namna wizi wake utakavyokwenda mpaka atakapofanikiwa. Pili mwizi huyu alikua na target. Alifahamu tokea mwanzo ni nini alikitaka kutoka kwa nani na akajipanga kukipata. Nadhani mwizi alitumia muda mwin...
Picha
Unaweza Kuwa Vile Unavyotaka Uamuzi Ni Wako Mara nyingi tumekuwa tukitamani kuwa watu wa aina fulani. Wakati mwingine tumetamani kuwa kama baadhi ya watu wenye mafanikio ambao wanatuvutia sana.  Lakini wengi wetu tunaishia kutamani tu bila kufikia pale tunapokusudia. Mara kwa mara tumeaminishwa kuwa watu wanaofikia mafanikio wamezaliwa na bahati, au wengi hutumia usemi wa Kiswahili kuwa “maji hufuata mkondo”. Wakiwa na maana kuwa kuna baadhi ya watu au familia ambazo wamejaliwa kuwa na mafanikio na wengine hawawezi kwakua hawana bahati hiyo. Ukweli ni kwamba kila mmoja wetu anaweza kufikia kiwango chochote kile cha mafanikio kama akiamua. Kuna baadhi ya kanuni ambazo zinatakiwa kufuatwa ili kufikia popote unapohitaji bila kujali rangi, kimo, kabila, ukoo wala taifa. Kama ambavyo ukifuata kanuni za kushindwa basi lazima utafikia kushindwa bila kujalisha wewe ni nani na unatokea wapi? Katika kila kiwango unachotaka kufikia, ni vizuri kufahamu kanuni na sheria za k...
Picha
Mambo Nane(8) Yatakayokufanya Uwe Na Fikra Chanya Kila Wakati Ili Uweze Kufikia Mafanikio Habari ndugu msomaji. Leo ningependa tuangalie namna ambavyo unaweza kujijenga na kuwa na fikra chanya kila wakati bila kujali watu wanaokuzunguka au matukio ambayo yametokea na kukuvunja moyo. Siri ya kuwa na mafanikio katika kila unalolifanya ni kuwa na fikra chanya. Ukishakuwa na fikra hasi tu, basi hata kukamilisha matamanio yako itakuwa ngumu. Ni dhahiri kuwa vile tunavyoviona nje vilianzia ndani yetu. Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana kujenga fikra chanya ili kuleta matokeo mazuri ya nje/katika ulimwengu wa mwili.  Tutaangalia baadhi ya vitu vitakavyotusaidia kutujengea fikra chanya na kama utakua na baadhi ya sababu ambazo unahisi kwako ni muhimu katika kukuongezea fikra chanya basi utaongezea na uweke katika karatasi ili kila ukiamka uzipitie, ili hali yoyote ile mbaya inapokukumba ukumbuke kuwa kuna mahala unaweza kusoma na ukarudi katika hali yako ya kawaida. 1.  Kuamka ...

Hivi ndivyo Unavyoweza Kujijengea Ujasiri na Kufanya Mambo Makubwa Zaidi Y a Unavyoweza Kufikiri

Hivi ndivyo Unavyoweza Kujijengea Ujasiri na Kufanya Mambo Makubwa Zaidi Y a Unavyoweza Kufikiri Nina imani umeshawahi kusikia au kusoma historia za watu tofauti tofauti na mara nyingine ukawaza kuwa watu hao walikua jasiri sana. Kuna watu mbalimbali waliowahi kuendesha nchi, kufanya vitu vya utofauti ambavyo kwa hali ya kawaida sio kila mtu anaweza kufanya, watu waliochukua maamuzi magumu ambayo sio rahisi kufikiria kwanini waliamua kuchukua maamuzi magumu kiasi hicho. Inawezekana wakati wanafanya maamuzi hayo hata watu wa karibu yao yaani ndugu na marafiki hawakuungana nao kwakua maamuzi hayo yalikuwa ni magumu mno, hivyo waliwakataza kufanya maamuzi hayo. Ukiwasoma au kuwasikia watu hawa unakubali kuwa watu hawa walikuwa na ujasiri mno. Inawezekana pia kwenye familia yako kuna mtu jasiri wa namna hii katika eneo fulani la maisha,je na wewe pia ungetamani kuwa  jasiri? Endelea kusoma makala hii mpaka mwisho na ufanyie kazi yale unayoyasoma kwa umakini ili uweze kuwa na ujasi...